Mfumo Wa Mashtaka Ufanane Nchi Nzima – Mpanju
HomeHabari

Mfumo Wa Mashtaka Ufanane Nchi Nzima – Mpanju

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju ataka mfumo wa mashtaka nchini uwe unaoeleweka, uliowazi na unaofanana n...


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju ataka mfumo wa mashtaka nchini uwe unaoeleweka, uliowazi na unaofanana nchi nzima.

Ndg. Mpanju ameyasema hayo leo June 21, 2021 jijini  Arusha wakati akifungua kikao kazi cha wadau kutoka sekta mbalimbali za haki jinai zilizokutana pamoja katika kikao cha siku tatu cha kupata maoni yatakayowezesha kuandaa sera ya taifa ya mashtaka nchini.

“Wadau wote muhimu wamehudhuria kikao hiki na nategemea mtashirikiana kuweka mfumo wa mashtaka unaoeleweka, uliowazi na unaofanana nchi nzima na kuandaliwa kwa sera hii ya taifa ya mashtaka haimaanishi kuwa itaingilia madaraka ya Mkurugenzi wa mashtaka nchini  na kushindwa kufanya majukumu yake” amesema.

Aliongeza kuwa madhumuni ya kukutana katika kikao kazi hicho ni kudadavua, kutoa mawazo na mapendekezo na kupitia sheria zilizowekwa za haki jinai ili kupata sera ya taifa ya haki jinai itakayotuvusha miaka kumi ijayo na kuweka vizuri mfumo wa haki jinai.

Naibu Katibu Mkuu huyo amewataka washiriki hao kushirikiana na kutumia utaalamu wao ili kupata sera inayotakiwa kwani sera hiyo ikikaa sawa haki za binadamu zitalindwa, mfumo wa haki jinai utaeleweka na wananchi watatii sheria.

Pia alisema, sera hii ya taifa ya mashtaka ikikaa vizuri itasaidia mfumo wa mashtaka nchini na maoni yatakayotolewa yatasambazwa kwenye taasisi zote za haki jinai ili kupata sera nzuri zaidi.

Awali akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu huyo kuongea na washiriki wa kikao, Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Ufuatiliaji Haki Bw. Patience Ntwina amewasisitiza washiriki hao kutoa mawazo yao ili kufanikisha kupatikana kwa sera ya taifa ya mashtaka iliyo bora na itakayosaidia mfumo wa haki jinai.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Mfumo Wa Mashtaka Ufanane Nchi Nzima – Mpanju
Mfumo Wa Mashtaka Ufanane Nchi Nzima – Mpanju
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiGyYCATsiAhAtP35xJ8GNIW7ClAKYrAE-Pc0KmLXbJdSWbqbdZV8awOq8Qj135G7A5C4cXCxhOHpUmGH-GA9WNh8KASoa8uvcmpYDXdaIawyZpL1mDQglL8-jGqqvZJlRgNRnke2yWV3cD/s16000/1.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiGyYCATsiAhAtP35xJ8GNIW7ClAKYrAE-Pc0KmLXbJdSWbqbdZV8awOq8Qj135G7A5C4cXCxhOHpUmGH-GA9WNh8KASoa8uvcmpYDXdaIawyZpL1mDQglL8-jGqqvZJlRgNRnke2yWV3cD/s72-c/1.jpeg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/mfumo-wa-mashtaka-ufanane-nchi-nzima.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/mfumo-wa-mashtaka-ufanane-nchi-nzima.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy