KIUNGO KUTOKA NIGERIA AKUBALI KUTUA SIMBA
HomeMichezo

KIUNGO KUTOKA NIGERIA AKUBALI KUTUA SIMBA

  U NAKUMBUKA  ule mchezo kati  ya Simba na  Plateau wa Ligi ya  Mabingwa Afrika kwenye  Uwanja wa Mkapa jijini Dar?  Basi kuna viungo waw...

CR 7 ANATAKA KUONDOKA JUVENTUS
MKUDE RUKSA KUJIUNGA YANGA, MKATABA WAKE SIMBA BADO
HASSAN KESSY AANDALIWA MKATABA YANGA

 UNAKUMBUKA ule mchezo kati ya Simba na Plateau wa Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar? Basi kuna viungo wawili wa Plateau United kutoka Nigeria walikichafua kweli pale katikati ya uwanja ambao ni Issa Ndala na Ochewechi Oche.

Kati ya hao basi fahamu kuwa kiungo mshambuliaji Ochewechi Oche amefunguka kuwa yupo katika mazungumzo ya awali na Klabu ya Simba ambao wameonyesha nia ya kumhitaji kiungo huyo.

 

Katika mchezo huo Simba ililazimishwa suluhu dhidi ya Plateau ambao ulikuwa mchezo wa mtoano wa awali kwa ajili ya kufuzu makundi na Simba kusonga mbele mara baada ya kuwa na faida ya ushindi wa bao 1-0 waliupata wakiwa ugenini nchini Nigeria.

 

Akizungumza na Championi Jumamosi moja kwa moja kutoka nchini Nigeria, Ochewechi Oche aliweka wazi kuwa yupo katika mazungumzo na Simba ambao walianza kuongea naye tangu kumalizika kwa mchezo wao walipokutana katika michuano ya kimataifa.

 

“Simba walinitafuta tangu tulipomaliza mchezo wa pili wa Ligi ya Mabingwa kule Tanzania, waliniambia msimu ukimalizika tutafanya mazungumzo na tayari kila kitu kuhusu mimi anakifahamu meneja wangu ambaye aliniambia kuwa wapo katika mazungumzo.

 

"Kwangu haina shida kujiunga Simba kwani ni timu nzuri na kubwa kwa Afrika, hivyo kama kila kitu kitakuwa sawa nipo tayari kujiunga na Simba,” alisema mchezaji huyo.

 

Naye meneja wa mchezaji huyo, Kunle Soname alithibitisha kuwa katika mazungumzo na Simba huku akiweka wazi kuwa viongozi wa Simba wapo siriazi na mchezaji huyo.

 

“Nipo katika mazungumzo na Simba ambao viongozi wameniambia kuwa wapo tayari kumsajili mchezaji wangu ila wameniambia wanasubiri mpaka msimu wa ligi yao umalizike, kwangu mimi pamoja na mchezaji ni jambo jema kuwa katika mazungumzo na moja kati ya timu kubwa Afrika na tutafurahi tukikamilisha dili hili,” alisema meneja huyo.

 

Kwa upande wake, msemaji wa timu hiyo, Albert Dakup alisema kuwa wamekuwa wakifuatilia Ligi ya Tanzania kwa karibu kwa kuwa wamepokea ofa ya kiungo wao kutakiwa na timu kubwa za Tanzania ikiwemo Simba.

 

“Najua ligi haijamalizika huko, tumekuwa tukifuatilia kwa karibu ligi ya Tanzania kwa sababu imekuwa na ushindani mkubwa hasa kwa timu ambazo zinakamata nafasi ya juu hasa Simba, Yanga na Azam.


“Kuhusu suala la Ochowechi ninachokijua ni kwamba tumepokea ofa kutoka kwa timu za huko licha ya kwamba Simba ndiyo imekuwa ikitajwa sana lakini zipo klabu nyingi ambazo zinahitaji kumpata, siwezi kukueleza ofa ya Simba ipoje ila inatajwa maana uongozi wa juu ndiyo unafahamu kila kitu ila bado hawajaweka wazi,” alisema Dakup.

 

Kutokana na ubora wa uchezeshaji wa Ochewechi Oche kama atafanikisha usajili wake wa kujiunga na Simba basi atacheza sambamba na kiungo mkabaji wa timu Thadeo Lwanga lakini atakumbana na upinzani mkali wa namba na wachezaji kama Mzamiru Yassin, Said Ndemla na Jonas Mkude ambao hucheza katika nafasi anayocheza yeye.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: KIUNGO KUTOKA NIGERIA AKUBALI KUTUA SIMBA
KIUNGO KUTOKA NIGERIA AKUBALI KUTUA SIMBA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjoFRxhyI0xyc6buF-YlYf2Eudwqh3nn4dzu6FAPycWjoVvLcPYEoyrVmx2XyqeHp47QXs6WlfwQ9XKxt2TlWXAolR9nXD_5LS0eBa_Zo57r0m-R-2LGGHeOJSwvIFnFUusVJcjshnhRd0T/w640-h426/Plateau+Mido.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjoFRxhyI0xyc6buF-YlYf2Eudwqh3nn4dzu6FAPycWjoVvLcPYEoyrVmx2XyqeHp47QXs6WlfwQ9XKxt2TlWXAolR9nXD_5LS0eBa_Zo57r0m-R-2LGGHeOJSwvIFnFUusVJcjshnhRd0T/s72-w640-c-h426/Plateau+Mido.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/kiungo-kutoka-nigeria-akubali-kutua.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/kiungo-kutoka-nigeria-akubali-kutua.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy