Jambazi Sugu Auwa Wakati Akijaribu Kuwatoka Polisi Shinyanga
HomeHabari

Jambazi Sugu Auwa Wakati Akijaribu Kuwatoka Polisi Shinyanga

SALVATORY NTANDU Mkazi wa mtaa wa Ndembezi manispaa ya Shinyanga anayetuhumiwa kuwa ni jambazi sugu, Idd Masasi (43) ameuawa kwa kupigwa...


SALVATORY NTANDU
Mkazi wa mtaa wa Ndembezi manispaa ya Shinyanga anayetuhumiwa kuwa ni jambazi sugu, Idd Masasi (43) ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi katika tukio la  majibizano ya risasi wakati akijaribu kuwatoroka polisi baada ya kukataa kujisalimisha kwa vyombo vya usalama.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani humo,kamishina msaidizi wa jeshi la polisi (ACP) Debora Magiligimba amethibitisha kutokea kwa tukio hilo  mei 31 mwaka huu na kusema kuwa Idd anatuhumiwa kufanya matukio ya uhalifu ya unyang’anyi wa kutumia silaha katika mikoa ya Shinyanga na Dar es salaam.

“Jeshi hilo lilipata taarifa za siri za uwepo wa jambazi (Idd Masasi) ambaye alikuwa anatafutwa na jeshi la polisi  makosa ya unyang’anyi wa kutumia silaha hasa matukio yaliyotokea hivi karibuni katika maeneo ya kigamboni na Dar es salaam na kisha kukimbilia mkoani Shinyanga,”alisema Magiligimba.

Alisema kuwa taarifa za kutafutwa kwake zilifunguliwa katika vituo vya Polisi kigamboni kwa kumbumbu za vitabu namba  KGD/IR/1050/2021, KGD/IR/411/2021 ambazo zilifunguliwa kwa lengo la kuendelea kumtafuta ili aweze kufikishwa kwa vyombo vya ulinzi na usalama baada kutoroka baada ya kutekeleza uhalifu huo.

“Baada ya kupata taarifa askari wetu  wakishirikiana na kikosi kazi cha askari kutoka jijini Dar es Salaam liliweka mtego maeneo ya soko la Nguzo Nane na ambapo majira ya saa tano alipofika katika eneo hilo na aligundua anafuatiliwa  alianza kukimbia ndipo askari walipompa ilani ya kusimama kwa kufyatua risasi hewani lakini alikaidi,”alisema Magiligimba

Kamanda Magiligimba amesema kuwa askari waliamua kumfyatulia risasi mbili bila kuleta madhara kwa watu wengine waliokuwepo eneo hilo, risasi hizo zilimjeruhi mguu wa kushoto na sehemu ya mgongoni na kisha  kumkamata na kupelekwa hospitali ya mkoa kwajili ya matibabu na alifariki dunia wakati anapatiwa matibabu.

“Nitoe onyo kwa waharifu wote kuwa mkoa wetu siyo sehemu rafiki ya kutenda uharifu au kukimbilia waharifu kujificha baada ya kufanya uharifu mikoa mingine kwani jeshi la polisi limejipanga vizuri kukabiliana nao, aidha mharifu yeyote atakayethubutu kufanya uharifu atakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria, waharifu wote wafahamu kwamba sehemu ambayo wapo na sisi jeshi la polisi tupo,” alisema Magiligimba

Kamanda Magiligimba amefafanua kuwa kumbukumbu za polisi zinaonyesha kuwa Idd alishawahi kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha mwaka 2011 na kutumikia adhabu hiyo katika gereza la Butimba, Mwanza na baadae alitoka kwa rufaa.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo kwa ajili ya uchunguzi.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Jambazi Sugu Auwa Wakati Akijaribu Kuwatoka Polisi Shinyanga
Jambazi Sugu Auwa Wakati Akijaribu Kuwatoka Polisi Shinyanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPC9Pr7xJtVOdANR87UTI48ASxpx-u8MAyEkJa3uarGWukM6lGQmUHlJRoFO5ePexHNah3sr3S9gocHboeBGvd97FhAcAeEbRoiy86voeH9r8Z1Dv7O4lV7UcyKVFNclDGTy1nEidJB7i4/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPC9Pr7xJtVOdANR87UTI48ASxpx-u8MAyEkJa3uarGWukM6lGQmUHlJRoFO5ePexHNah3sr3S9gocHboeBGvd97FhAcAeEbRoiy86voeH9r8Z1Dv7O4lV7UcyKVFNclDGTy1nEidJB7i4/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/jambazi-sugu-auwa-wakati-akijaribu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/jambazi-sugu-auwa-wakati-akijaribu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy