IGP Sirro afanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa Jeshi la Polisi
HomeHabari

IGP Sirro afanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa Jeshi la Polisi

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Simon Sirro amefanya mabadiliko madogo kwa Makamanda wa Polisi, ili kujaza nafasi zilizoachwa wazi. Kati...


Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Simon Sirro amefanya mabadiliko madogo kwa Makamanda wa Polisi, ili kujaza nafasi zilizoachwa wazi.

Katika mabadiliko hayo, .Naibu Kamishna wa Polisi Lucas Mkondya amehamishwa kutoka kuwa Kaimu Kamishna wa Fedha na Logistiki Makao Makuu ya Polisi Dodoma kuwa Mkuu wa Usalama Barabarani nchini na Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kipolisi Rufiji, – Onesmo Lyanga amehamishwa kwenda kuwa Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma kuchukua nafasi ya Kamanda Gilles Muroto ambaye anastaafu.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ramadhan Ngh’anzi amehamishwa kutoka kuwa Boharia Mkuu kwenda kuwa Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, huku Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Mwamini Rwantale akihamishwa kutoka Kanda Maalum ya Dar es Salaam ambako alikuwa Mkuu wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali watu kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Tazara.

IGP Sirro pia amemhamisha Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mwanza, – Muliro Jumanne kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kuchukuwa nafasi iliyoachwa na Kamishna wa Polisi Camillius Wambura.

Kamishna Msaidizi wa Polisi Zuberi Chembera, yeye amehamishwa kutoka Makao Makuu ya Upelelezi Dodoma kwenda Makao Makuu ya Polisi Zanzibar kuwa Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa jinai Zanzibar kuchukua nafasi ya Kamishna wa Polisi Hamad Khamis Hamad.

Naye Kamishna Msaidizi wa Polisi Stella Richard amehamishwa kutoka kuwa Kamanda wa Kikosi cha Polisi Tazara kwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: IGP Sirro afanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa Jeshi la Polisi
IGP Sirro afanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa Jeshi la Polisi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhqR3g6QjFJuzZM5PjvIb17ymgvX-UDSDi2SyRey38kl9vwh7pa7MgmgkJsTKbLWBJZ7D7RzpgI5oI8v8c50_6hCnSTH8rWr-Vnvc-psJjD-4QMdrbfjuu9oTyjK1O-we-5mFifSGqJ_css/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhqR3g6QjFJuzZM5PjvIb17ymgvX-UDSDi2SyRey38kl9vwh7pa7MgmgkJsTKbLWBJZ7D7RzpgI5oI8v8c50_6hCnSTH8rWr-Vnvc-psJjD-4QMdrbfjuu9oTyjK1O-we-5mFifSGqJ_css/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/igp-sirro-afanya-mabadiliko-kwa-baadhi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/igp-sirro-afanya-mabadiliko-kwa-baadhi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy