SUALA LA UBINGWA WA LIGI KUU BARA, YANGA WAFUNGUKA
HomeMichezo

SUALA LA UBINGWA WA LIGI KUU BARA, YANGA WAFUNGUKA

  N AHODHA msaidizi  wa kikosi cha  Yanga, Bakari  Mwamnyeto  amesema kuwa licha ya  timu hiyo kuwa na matokeo  yasiyotabirika katika  mic...


 NAHODHA msaidizi wa kikosi cha Yanga, Bakari Mwamnyeto amesema kuwa licha ya timu hiyo kuwa na matokeo yasiyotabirika katika michezo ya hivi karibuni, bado hawajakata tamaa katika malengo yao ya kutwaa ubingwa msimu huu.


Yanga,Jumatano waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya JKT Tanzania na kufikisha pointi 61, hivyo kuwafikia vinara wa msimamo wa Ligi Kuu Bara, Simba ambao wamejikusanyia pointi 61 licha ya kuwa na michezo minne pungufu dhidi ya Yanga.

 

Yanga wamekuwa na mwenendo wa kusuasua ambapo katika michezo nane mfululizo iliyopita wamefanikiwa kushinda michezo mitatu pekee, wamepoteza miwili na kutoa sare kwenye tatu.


Matokeo hayo yameonekana kuzidi kuwapunguza kasi Yanga katika vita ya kuwania ubingwa wa msimu huu.

 

Akizungumzia mipango yao Mwamnyeto alisema: “Ni kweli tumekuwa na mwendo wa kusuasua kwenye michezo yetu iliyopita, lakini tunaamini kuwa hiyo ni hali ya kawaida na ni suala ambalo tayari linafanyiwa kazi na benchi letu la ufundi.

 

"Hivyo, tunapambana kuhakikisha tunafikia malengo yetu msimu huu ikiwemo kumaliza katika nafasi za juu, na hata kutwaa ubingwa.”


Naye Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli akizungumza na Championi Ijumaa, alisema:

 

“Tunaendelea kujenga kikosi chetu, lakini pia tunaendelea kupigania malengo yetu ya kutwaa ubingwa msimu huu, changamoto ya matokeo ni kitu cha kawaida na hatuwezi kukata tamaa.”





Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: SUALA LA UBINGWA WA LIGI KUU BARA, YANGA WAFUNGUKA
SUALA LA UBINGWA WA LIGI KUU BARA, YANGA WAFUNGUKA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidbsZ1afcdSbeXzvHNRnFyE7tOE7botsJDiLpxoHjKlwVyOTF63j3BmB9kVqxxbZLTMRHD55RjQC5vYGmOwd2k4UtnXYAWXWwS62kBlbS8EFmkP0CRzRK-gBx63RUjjnWr3NMP4GULWg1t/w640-h530/Kikosi+cha+Yanga+2020.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidbsZ1afcdSbeXzvHNRnFyE7tOE7botsJDiLpxoHjKlwVyOTF63j3BmB9kVqxxbZLTMRHD55RjQC5vYGmOwd2k4UtnXYAWXWwS62kBlbS8EFmkP0CRzRK-gBx63RUjjnWr3NMP4GULWg1t/s72-w640-c-h530/Kikosi+cha+Yanga+2020.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/suala-la-ubingwa-wa-ligi-kuu-bara-yanga.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/suala-la-ubingwa-wa-ligi-kuu-bara-yanga.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy