Majaliwa: Tutumie Mweziwa Ramadhani Kumuomba Mwenyezi Mungu Aendelee Kuibariki Tanzania
HomeHabari

Majaliwa: Tutumie Mweziwa Ramadhani Kumuomba Mwenyezi Mungu Aendelee Kuibariki Tanzania

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasisiza waislam nchini watumie Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kwa kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuibariki T...

Bandari ya Tanga sasa inashughulikia meli kubwa baada umya uwekezaji wa Bilioni 429
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo October 20, 2024
Gabon inatarajiwa kupiga kura ya maoni kuhusu katiba mpya Nov 16


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasisiza waislam nchini watumie Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kwa kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuibariki Tainzania, viongozi na wananchi wake wadumishe amani na mshikamano.

Ameyasema hayo jana(Jumapili, Mei 2, 2021) katika Fainali za Mashindano ya 29 ya Kimataifa ya Qur’an yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yahusisha washiriki 15 kutoka nchi 11.

Pia, Waziri Mkuu ametoa rai kwa waumini wa dini ya kiislam nchini waendelee kuyaishi mafundisho wanayoyapata katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kwenye maisha yao ya kila siku.

 “Natambua mchango mkubwa wa waumini katika kuienzi na kuitunza amani kwa kufuata miongozo ya viongozi wetu kupitia mafundisho ya Qur’an ambayo hututaka kuepuka kuivuruga amani.”

Amesema amani ni matokeo ya msingi imara iliyoachwa na waasisi wa Taifa, hivyo hawana budi kuienzi na kuilinda kwa ajili ya maslahi na mustakabali wa nchi. “Mwitikio mkubwa tunaouona kwenye mashindano haya ni kielelezo cha amani, umoja na mshikamano tulionao.”

Pia, Waziri Mkuu amesema ni vema vijana hao waliohifadhi Qur’an wakaendelezwa kitaaluma katika fani zingine za elimu kwani uwepo wao ni muhimu katika kujenga jamii bora na yenye uadilifu.

Amesema si jambo rahisi kumuona mtaalamu aliyehifadhi qur’an akienda kinyume na maadili ya taaluma yake kwa sababu Qur’an pekee inatosha kumfanya mwanataaluma huyo aonyeke dhidi ya vitendo vinavyokwenda kinyume na uadilifu.

Waziri Mkuu ametoa wito kwa wadau mbalimbali waunge mkono juhudi zinazofanywa na taasisi mbalimbali za kuhifadhisha Qur’an nchini katika kujenga Taifa bora la vijana wenye maadili na kutoa wataalamu wa fani mbalimbali ambao wana hofu ya Mwenyezi Mungu katika mioyo yao.

Kwa upande wake, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zuber ametumia fursa hiyo kuwahamasisha waumini wa dini ya kiislam kujenga utamaduni wa kuhifadhi Qur’an kwa kuwa ndiyo jambo muhimu kwa sasa.

Awali, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kuhifadhisha Qur’an Tanzania, Sheikh Othman Kaporo aliziomba  taasisi mbalimbali za kiislaam kushirikiane katika kuwalea vijana kwenye maadili mema.

Katika mashindano hayo mshiriki kutoka nchini Yemen, Mohammed Abdo Ahmed (22) ameshinda nafasi ya kwanza katika upande wa kuhifadhi qur’an na amepata zawadi ya Dola za Marekani 5,000 na Mohammed Haruna Hassani (37) ameshika nafasi ya kwanza kwa upande wa kusoma Qur’an kwa njia ya tajweed na kupewa zawadi ya shilingi milioni mbili.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Majaliwa: Tutumie Mweziwa Ramadhani Kumuomba Mwenyezi Mungu Aendelee Kuibariki Tanzania
Majaliwa: Tutumie Mweziwa Ramadhani Kumuomba Mwenyezi Mungu Aendelee Kuibariki Tanzania
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhSJgeVIT7tda7ZTshj_LPWWsEdC2xs4-SAuucMjicQAkwZ2Nq92R6oJatH5TWiqDS2urt9wzaWii9XLujLHkhxfn5pNr7njPbxE7wnKw_ja5uhtfMyrld9Nv3fR4qVEEaxfIDDefC_Rqxq/s16000/1.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhSJgeVIT7tda7ZTshj_LPWWsEdC2xs4-SAuucMjicQAkwZ2Nq92R6oJatH5TWiqDS2urt9wzaWii9XLujLHkhxfn5pNr7njPbxE7wnKw_ja5uhtfMyrld9Nv3fR4qVEEaxfIDDefC_Rqxq/s72-c/1.jpeg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/majaliwa-tutumie-mweziwa-ramadhani.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/majaliwa-tutumie-mweziwa-ramadhani.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy