KIPA NAMBA MOJA WA SIMBA MANULA AFUATWA NA WAARABU
HomeMichezo

KIPA NAMBA MOJA WA SIMBA MANULA AFUATWA NA WAARABU

  W AKATI kipa  wa Simba,  Aishi Manula  akiendelea  kung’ara  kwenye michuano ya Ligi  ya Mabingwa Afrika  Rais wa Klabu ya  Al-Merrikh ...

KOCHA WA YANGA ATAKA MECHI TATU KUWAWAKE FITI VIJANA WAKE
MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA ALHAMISI
VIDEO: AJIBU ANUKIA KUTUA YANGA, GOMES AJIPA MECHI TANO KUTWAA UBINGWA

 


WAKATI kipa wa Simba, Aishi Manula akiendelea kung’ara kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika Rais wa Klabu ya Al-Merrikh SC ya Sudan, Adam Sudacal yupo tayari kutoa ofa ya zaidi ya Sh milioni 230 ili amweze kuinasa saini ya kipa huyo.


Manula bado yupo kwenye mkataba na Klabu ya Simba anaonekana kusakwa na miamba hiyo ya Sudan, baada ya kutengeneza rekodi ya kutofungwa bao lolote katika michezo ya Kundi A kati ya minne ambayo timu yake imecheza.

 

Awali mchezo wake wa kwanza katika hatua hiyo kusimama langoni ni dhidi ya AS Vita wakiwa ugenini wakashinda bao 1-0, wa pili ni dhidi ya Al Ahly ya Misri uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa, Darambapo Simba ilishinda kwa bao 1-0 lililofungwa na Luis Miquissone.

 

Mchezo wa tatu dhidi ya Al-Merrikh wakiwa ugenini hakucheza kwa kuwa hakuwa fiti kiafya na nafasi yake ikachukuliwa na Beno Kakolanya, matokeo yakiwa 0-0


Manula alisimama langoni katika mchezo wa nne dhidi ya Al-Merrikh akiokoa michomo kadhaa ambayo wapinzani walipata nafasi za wazi kwenye Uwanja wa Mkapa, Simba ikishinda kwa mabao 3-0.


Habari zinaeleza kuwa inaonekana harakati za Kocha Mkuu wa Al-Merrikh ya Sudan, Lee Clark anaitaka zaidi saini ya Manula ili aendelee kukiboresha kikosi hicho jambo ambalo linadaiwa kuwafanya miamba hiyo kuzidi kupambana kumpata kipa huyo.

 

“Naomba nikwambie tu kuwa ni kweli nilisikia Manula kama anauliziwa na Waarabu flani hivi, ila kwa kuwa sikuwa na wazo lolote juu ya kutakiwa na jamaa hao kiukweli sikufatilia alichokuwa anatafutiwa.

 

“Isipokuwa nakumbuka nilikutana na mmoja wa wachezaji hapa, akaniambia naona dili la Aishi kwa Wasudan linaelekea ukingoni, nilipomuuliza kwa nini ndiyo akaniambia kuwa kuna jamaa kutoka Sudan walienda kumuona kwenye mechi ya Stars na Equatorial Guinea,” kilisema chanzo hicho.

 

Hivi karibuni kulikuwa na hizo taarifa kuwa Al-Merrikh imekuwa na mpango huo wa kumuwania Manula jambo ambalo muda wowote endapo Simba kupitia kwa mwekezaji wao, Mohamed Dewji ‘Mo’ watakubaliana nao juu ya ofa yao waliyotoa wakimtaka aende kujiunga na kikosi chao, inaweza kuwa dili zuri.

 

Lakini kwa upepo ulivyo, halitakuwa jambo jepesi kwa Simba kumruhusu mchezaji huyo kuondoka kwa kuwa wamekuwa wakiimarisha usajili wao ili kuwa bora katika ngazi ya kimataifa.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: KIPA NAMBA MOJA WA SIMBA MANULA AFUATWA NA WAARABU
KIPA NAMBA MOJA WA SIMBA MANULA AFUATWA NA WAARABU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUt7lNJ2aYAIL3gGX0UamlmgnmRqlPpYnPxnVEEmkLkIu-tmrpXidKZKQzLvU8Q9XdRf_xJu8ArRWeGqFrmnjoTfksSZZNcZKHrhXsKnEUh95DcyYe3IFH_lI6fWxS7LZh3YTyRMnK3vXA/w640-h360/Manula+v+Yanga.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUt7lNJ2aYAIL3gGX0UamlmgnmRqlPpYnPxnVEEmkLkIu-tmrpXidKZKQzLvU8Q9XdRf_xJu8ArRWeGqFrmnjoTfksSZZNcZKHrhXsKnEUh95DcyYe3IFH_lI6fWxS7LZh3YTyRMnK3vXA/s72-w640-c-h360/Manula+v+Yanga.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/kipa-namba-moja-wa-simba-manula-afuatwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/kipa-namba-moja-wa-simba-manula-afuatwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy