Kamati Ya Bunge Yapongeza Jitihada Za Wizara Kuzalisha Mbegu Za Mazao
HomeHabari

Kamati Ya Bunge Yapongeza Jitihada Za Wizara Kuzalisha Mbegu Za Mazao

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo ,Mifugo na Maji imepongeza jitihada za wizara ya kilimo kuzalisha mbegu bora za mazao ya kilimo kupit...


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo ,Mifugo na Maji imepongeza jitihada za wizara ya kilimo kuzalisha mbegu bora za mazao ya kilimo kupitia Wakala wa Taifa wa Mbegu (ASA)

Hayo yameelezwa jana Morogoro (15.03.2021) na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Christine Ishengoma alipoongoza wajumbe kukagua utendaji kazi wa Wakala wa Mbegu nchini (ASA) pamoja na  ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu (TOSCI).

"Tunapongeza wakala wa mbegu ASA kwa kushika nafasi ya tano kati ya makampuni 42 yanayozalisha mbegu  ambapo kwa mwaka 2019/20 ilizalisha tani 1,750 za mazao mbalimbali" alisema Dkt.Ishengoma.

Naye Mtendaji Mkuu wa ASA Dkt. Sophia Kashenge akiwasilisha taarifa kwa kamati ya kudumu ya Bunge alisema kwa kushirikiana na makampuni manane wamefanikiwa kuzalisha mbegu kwenye mashamba ya serikali toka tani 3,450 mwaka 2016/17 hadi tani 5,634 mwaka 2019/20.

Dkt.Kashenge aliongeza kusema katika kipindi cha miaka minne iliyopita wakala umefanikiwakuzalisha miche 342,000 ya michikichi ambapo miche 10,200 tayari imegawiwa bure kwa wakulima kwenye wilaya nne za Mkoa wa Kigoma kama ilivyoagizwa na Waziri Mkuu.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Prof.Adolf Mkenda alisema ili kuhakikisha nchi inafikia utoshelevu wa uzalishaji mbegu za mazao ya kilimo atazikutanisha taasisi za ASA,TOSCI na TARI ili kujadili na kuweka mkakati wa pamoja wa kitaalam kuwezesha upatikanaji wa mbegu bora nyingi.

Prof. Mkenda aliwashukuru wabunge kwa kutembelea taasisi hizo zenye kazi kubwa ya kuhakikisha nchi inajitosheleza kwa uzalishaji mbegu na kuwa katika bajeti ijayo 2021/22 wizara itaomba Bunge kupitisha makadirio ya bajeti ili sekta ya mbegu ipate fedha za kutosha.

Takwimu zinaonesha katika kipindi cha miaka minne upatikanaji wa mbegu umeongezeka kutoka tani 36,614 mwaka 2015/16 hadi tani 76,725 mwaka 2019/20 huku uzalishaji wa ndani wa mbegu bora umeongezeka kutoka tani 20,604 mwaka 2015/16 hadi tani 69,173 mwaka 2019/20.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Kamati Ya Bunge Yapongeza Jitihada Za Wizara Kuzalisha Mbegu Za Mazao
Kamati Ya Bunge Yapongeza Jitihada Za Wizara Kuzalisha Mbegu Za Mazao
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhOjy0w5UIpYDoGsph8-G7I9nay6M9DrlpDLXT_OWObo6zgzmnWbQxa5ibVp1Gbe9m3u8OMJumrq3I9GOu3sCYdPffGxALcxGrS7MqqfSFJ-OVq_m7Ec7dvw8pyHtj3shwxgijDpOVjhnRA/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhOjy0w5UIpYDoGsph8-G7I9nay6M9DrlpDLXT_OWObo6zgzmnWbQxa5ibVp1Gbe9m3u8OMJumrq3I9GOu3sCYdPffGxALcxGrS7MqqfSFJ-OVq_m7Ec7dvw8pyHtj3shwxgijDpOVjhnRA/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/kamati-ya-bunge-yapongeza-jitihada-za.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/kamati-ya-bunge-yapongeza-jitihada-za.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy