ISHU YA SIMBA KUPEWA POINTI TATU ZA AL MERRIKH IPO HIVI
HomeMichezo

ISHU YA SIMBA KUPEWA POINTI TATU ZA AL MERRIKH IPO HIVI

  BAADA ya uongozi wa Simba kupitia kwa Mtendaji Mkuu, Barbara Gonzalez kuandika barua kwa Shirikisho la Soka Afrika, (Caf) kuomba ufafan...

 


BAADA ya uongozi wa Simba kupitia kwa Mtendaji Mkuu, Barbara Gonzalez kuandika barua kwa Shirikisho la Soka Afrika, (Caf) kuomba ufafanuzi juu ya wachezaji wawili wa Al Merrikh waliocheza mchezo dhidi yao wakiwa wamefungiwa imeelezwa kuwa majibu yametolewa kwamba wachezaji hao hawana makosa.

Wachezaji hao wawili ambao ni Ramadhan Agab na Bakhit Khamis walicheza Machi 6, Uwanja wa Al Hilal kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, hatua ya makundi na ulikamilika kwa sare ya bila kufungana.

Habari zillieleza kuwa wachezaji hao wawili walikuwa wamefungiwa kucheza kwa kuwa kulikuwa na makosa kwenye mikataba yao  jambo ambalo liliwafanya Simba kuhitaji ufafanuzi kutoka Caf.

Endapo ingebainika kwamba wachezaji hao walicheza kwa makosa kwenye mchezo huo basi Simba ingepewa pointi tatu za mezani na kuifanya ifikishe pointi 9 kwa kuwa ilikuwa ina pointi sita kabla ya kucheza nao na wakati huu ina pointi 7.

Taarifa zimeeleza kuwa Caf wamewaambia Simba kwamba wachezaji hao walikuwa wamefungiwa kucheza ligi ya Sudan lakini wanaweza kucheza mashindano yanayosimamiwa na Caf.

Hivyo kwa taarifa hiyo ni kwamba kesho wachezaji hao watakuwa sehemu ya kikosi kitakachomenyana na Simba, Uwanja wa Mkapa kusaka pointi tatu na Simba haitapata pointi tatu.

Al Merrikh ikiwa kundi A inaonekana inaweza kuwa kikwazo kwa Simba kesho kwa kuwa ina pointi moja na kundi lipo wazi ikiwa itashinda kesho itafufua matumaini ya kufuzu robo fainali.

Pia ilifanya mabadiliko kwenye benchi la ufundi jambo linalowafanya waje na mbinu mpya kusaka ushindi hivyo lazima Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes kujipanga kusaka pointi tatu.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: ISHU YA SIMBA KUPEWA POINTI TATU ZA AL MERRIKH IPO HIVI
ISHU YA SIMBA KUPEWA POINTI TATU ZA AL MERRIKH IPO HIVI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhrxZLzvFQ79jwYo74YlFZW6N70fFzJtvq4aA0iIaY-_SUOvDEQ4xBrUuQFbxpYjzEkqUs2upoCeNki9MSQlNtdtcoIIcqeXSwmpoe8gHluA5AVvdxal0zUxcAOp7iXrzQFGXBWYxv84A71/w640-h426/Al+Merikh.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhrxZLzvFQ79jwYo74YlFZW6N70fFzJtvq4aA0iIaY-_SUOvDEQ4xBrUuQFbxpYjzEkqUs2upoCeNki9MSQlNtdtcoIIcqeXSwmpoe8gHluA5AVvdxal0zUxcAOp7iXrzQFGXBWYxv84A71/s72-w640-c-h426/Al+Merikh.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/ishu-ya-simba-kupewa-pointi-tatu-za-al.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/ishu-ya-simba-kupewa-pointi-tatu-za-al.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy