AZAM FC: MAGUFULI AMEFANYA MAKUBWA, ATAKUMBUKWA
HomeMichezo

AZAM FC: MAGUFULI AMEFANYA MAKUBWA, ATAKUMBUKWA

 UONGOZI wa Azam FC umeweka wazi kuwa bado heshima ya Rais wa awamu ya tano, John Pombe Magufuli itazidi kuishi kutokana na mambo makubwa ...

KIKOSI CHA MTIBWA SUGAR KINACHOTARAJIWA KUANZA LEO DHIDI YA YANGA
KIKOSI CHA YANGA KINACHOTARAJIWA KUANZA LEO DHIDI YA MTIBWA SUGAR
DK MSOLLA ANAKUMBUSHWA MAKOSA WAKATI AKIWA PEMBENI YA USUKANI….

 UONGOZI wa Azam FC umeweka wazi kuwa bado heshima ya Rais wa awamu ya tano, John Pombe Magufuli itazidi kuishi kutokana na mambo makubwa ambayo ameyafanya kwa taifa la Tanzania.

Maguli aliyetangulia mbele za haki Machi 17,2021, Machi 26 alipumzishwa kwenye makazi yake ya milele, Chato mkoani Geita katika makaburi ya familia ya Magufuli.

Kuondoka kwake kumeacha simanzi kwenye mioyo ya Watanzania pamoja na Waafrika kwa sababu alikuwa ni mtetezi wa wanyonge, mpenda haki bila kusahau kutekeleza majukumu yake kwa wakati.

Furaha yake kwenye michezo ilikuwa ni kuona timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars inashinda huku kwa timu zinazoshiriki Ligi Kuu Bara maono yake ilikuwa ni kuona kwamba siku moja timu moja inatwaa Kombe la Afrika, (Ligi ya Mabingwa Afrika).

Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit, amesema kuwa Magufuli alikuwa ni kiongozi shujaa na mwenye msimamo katika kusimamia kile anachokiamini.

"Magufuli alikuwa ni kiongozi makini na mwenye msimamo, atakumbukwa kwa kuwa mengi aliyokuwa akiyafanya yanaonekana na yanaleta matokeo kwa kila Mtanzania.

"Ukianza na kuruhusu kuanza kwa michezo mapema kwa timu zote za bara la Afrika haikuwa jambo jepesi ila aliamini inawezekana wakati ule wa janga la Corona.

"Tanzania ilikuwa ni nchi ya kwanza kuruhusu mashabiki kuingia uwanjani na mechi zikaendelea kama kawaida ambapo kuna mataifa mengine yalifuta ligi zao na nyingine zilisismamisha ligi kwa muda mrefu na ziliporudi mashabiki hawakuruhusiwa kuingia," amesema.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: AZAM FC: MAGUFULI AMEFANYA MAKUBWA, ATAKUMBUKWA
AZAM FC: MAGUFULI AMEFANYA MAKUBWA, ATAKUMBUKWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgpVleODM0NbpqCRTOI9A8IkCpla26qZQXHUWeFj7076Fo_dVsp-brS1RXEmhervWEf12ci1rFKQH8vsw0SgKlGYLakj9G7jK1Ai5wqUH-Q4hOtGbAqbPuDwZhCz38MuegByTZR6E34HlbS/w640-h360/magutena.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgpVleODM0NbpqCRTOI9A8IkCpla26qZQXHUWeFj7076Fo_dVsp-brS1RXEmhervWEf12ci1rFKQH8vsw0SgKlGYLakj9G7jK1Ai5wqUH-Q4hOtGbAqbPuDwZhCz38MuegByTZR6E34HlbS/s72-w640-c-h360/magutena.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/azam-fc-magufuli-amefanya-makubwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/azam-fc-magufuli-amefanya-makubwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy