YANGA KUPELEKWA FIFA NA SIBOMANA,KISA MKWANJA
HomeMichezo

YANGA KUPELEKWA FIFA NA SIBOMANA,KISA MKWANJA

PATRICK Sibomana ameibuka na kudai yupo kwenye mpango wa kuifungulia mashitaka Klabu ya Yanga kwenye Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa...


PATRICK Sibomana ameibuka na kudai yupo kwenye mpango wa kuifungulia mashitaka Klabu ya Yanga kwenye Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), kwa kile alichokieleza kuwa, ukiukwaji wa makubaliano ya malipo ya stahiki zake.

 

Hii inakuja ikiwa ni siku chache baada ya Fifa kuitaka Yanga kumlipa aliyekuwa mshambuliaji wa timu hiyo, Amissi Tambwe.

 

Sibomana ambaye ni mshambuliaji aliichezea Yanga kwa msimu uliopita kabla ya kuachwa mwishoni mwa msimu huo.


Nyota huyo anayeumia zaidi mguu wa kushoto amesema: “Tulikubaliana kwamba Yanga wanilipe fedha zangu za usajili ambazo zilibaki kiasi cha dola 10,000 (Sh mil 23).

 

“Kwa kuwa niliishi nao vizuri na nilijua timu ilikuwa haina fedha, tulipanga wanilipe kwanza fedha ya miezi mitatu pamoja na fedha ya usajili ambayo jumla yake ni dola 16,000 (Sh mil 36.9) ambayo nilikatwa hadi kufikia dola 14,500 (Sh mil 33.4).



“Tukakubaliana kwamba wangenilipa Oktoba 30, mwaka jana ambapo walinipatia dola 3,000 (Sh mil 6.9) ikabaki dola 11,500 (Sh mil 26.5) ambapo niliwaambia wanipatie zote, lakini cha kushangaza walinitumia dola 1,500 (Sh mil 3.4) na mwezi Januari mwaka huu wakanipatia pesa iliyobaki, ambapo deni likabaki dola 4,000 (Sh mil 9.2.

 

“Sasa mimi nilikwazika kwa sababu walikuwa wakinilipa kwa muda wanaotaka na kwa kiwango wanachotaka, kila nikiwatafuta viongozi wamekuwa wakiniambia kwa nini nawaandikia barua mara kwa mara, wakati inawezekana nikarejea kwao siku moja.

 

"Mimi naona wananionea, kwa kutofuata makubaliano tuliyokuwa nayo na sijui kwa nini? Hivyo kwa sasa tayari nimewaandikia barua Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), na kama suala langu litakuwa halijapatiwa ufumbuzi hadi kufikia Machi 1, basi sitakuwa na njia nyingine zaidi ya kupeleka malalamiko yangu Fifa.


“Kiukweli nisingependa kufika huko, lakini nadhani wao ndiyo wananisukuma kufanya hivyo,” amesema Sibomana.

 

Alipotafutwa Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Haji Mfikirwa azungumzie ishu hiyo alisema: “Taarifa kuhusiana na madai ya Sibomana tunazo hivyo tunashughulikia.".

 

Ulipotafutwa uongozi wa TFF kuthibitisha taarifa hiyo, Ofisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo amesema: “Kwa upande wangu siwezi kusema lolote kwa sasa mpaka pale nitakapopata nafasi ya kuwasiliana na kamati ya sheria kuhusiana na hilo. 



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: YANGA KUPELEKWA FIFA NA SIBOMANA,KISA MKWANJA
YANGA KUPELEKWA FIFA NA SIBOMANA,KISA MKWANJA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjq0syk-sgYxEQRSKQ7byg7EwazxE1PLq47EWrv2qIJYspGS5GihLkOQJF1MZaH8Eri6HBhqO0SvopWOHQ-hZhduCecNHDnhYuMJkyhfNwqW2-EruiD7IXzJxvWO5TqBjyPAgTaG_58JzIm/w640-h598/majembe.PNG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjq0syk-sgYxEQRSKQ7byg7EwazxE1PLq47EWrv2qIJYspGS5GihLkOQJF1MZaH8Eri6HBhqO0SvopWOHQ-hZhduCecNHDnhYuMJkyhfNwqW2-EruiD7IXzJxvWO5TqBjyPAgTaG_58JzIm/s72-w640-c-h598/majembe.PNG
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/yanga-kupelekwa-fifa-na-sibomanakisa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/yanga-kupelekwa-fifa-na-sibomanakisa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy