TPC Ongezeni Matumizi Ya Tehama Kuhudumia Wateja
HomeHabari

TPC Ongezeni Matumizi Ya Tehama Kuhudumia Wateja

Na Prisca Ulomi, WMTH Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Faustine Ndugulile ameuelekeza uongozi wa Shirika la Posta Tanz...


Na Prisca Ulomi, WMTH
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Faustine Ndugulile ameuelekeza uongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) kuongeza matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja.

Dkt. Ndugulile ameyasema hayo leo wakati akifungua mkutano wa 27 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania lililofanyika Dodoma.  Amefafanua kuwa hivi sasa dunia ipo kiganjani na inatumia TEHAMA na maisha yanakwenda kidijitali hivyo TPC nayo iongeze matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika kuhudumia wateja kwa kuwa kwa kufanya hivyo TEHAMA itaongeza mapato ya Shirika na kuongeza gawio lake kwa Serikali.

“Sitarajii kuona TPC inaendeshwa kwa hasara, tumieni rasilimali za Shirika kwa ajili ya ustawi wa Shirika na sio ustawi wa mtu binafsi”, amesisitiza Dkt. Ndugulile.

Aidha, amepongeza TPC kwa utendaji kazi wao na ametaka mfanyakazi mmoja mmoja wa TPC kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kila kiongozi wa Shirika kusimamia vizuri eneo lake la kazi na kutekeleza majukumu yake.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa Baraza ni chombo muhimu sana maeneo ya kazi na lipo kisheria na kwa hali ninayoiona hapa inaonekana kweli amani imetawala na kuna ushirikiano baina ya wafanyakazi na viongozi wa TPC na naamini kwa uongozi wako kwenye Wizara hii mpya tutahakikisha TPC inasimama imara katika kuhudumia wateja kwa kuwa tuna kiu ya kuona Shirika hili linakimbia.

Naye Postmasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Hassan Mwang’ombe amesema kuwa wajumbe wa Baraza hilo watakuwa na kikao cha siku tatu ambapo watajadili mapendekezo ya mpango wa maendeleo wa Shirika kwa mwaka 2021/2022; matumizi ya mifumo mipya ya kidigitali kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli za kila siku; sheria ya utumishi wa umma, wajibu na haki za kila mfanyakazi na kujadili maslahi ya wafanyakazi; mahusiano mahala pa kazi; na nidhamu katika utendaji kazi.

Kikao hicho kimejumuisha Menejimenti ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo; Dkt. Jim Yonazi; Mameneja wa TPC wa Mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar na viongozi wa vyama vya Wafanyakazi wa Shirika hilo.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: TPC Ongezeni Matumizi Ya Tehama Kuhudumia Wateja
TPC Ongezeni Matumizi Ya Tehama Kuhudumia Wateja
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhZrFVH4RUiJ_PPhb9gpwwG2bOOw-UtggqhPFQzAyex4OMuEuBMy3XHCH1w7kKE8WDvyD1x_fFpoR3yiKB9hxaCZErna51ORbigtsUQToM8YBEe0ZL7syYtdOHzC-B5fl_MwtnxZhmcoe4s/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhZrFVH4RUiJ_PPhb9gpwwG2bOOw-UtggqhPFQzAyex4OMuEuBMy3XHCH1w7kKE8WDvyD1x_fFpoR3yiKB9hxaCZErna51ORbigtsUQToM8YBEe0ZL7syYtdOHzC-B5fl_MwtnxZhmcoe4s/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/tpc-ongezeni-matumizi-ya-tehama.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/tpc-ongezeni-matumizi-ya-tehama.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy