Rais Magufuli Awasisitiza Wananchi Kulima, Kuchapa Kazi...."Usiyefanya kazi usile, hakuna cha bure"
HomeHabari

Rais Magufuli Awasisitiza Wananchi Kulima, Kuchapa Kazi...."Usiyefanya kazi usile, hakuna cha bure"

Rais John Magufuli, amesema hatasita kuwaondoa mara moja wakuu wa wilaya zote ambao maeneo yao yatakumbwa na njaa mwaka huu. Aidha, amet...


Rais John Magufuli, amesema hatasita kuwaondoa mara moja wakuu wa wilaya zote ambao maeneo yao yatakumbwa na njaa mwaka huu.
Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuzitumia mvua zinazoendelea kunyesha kwenye maeneo yao kwa kulima mazao ya aina tofauti.

Rais Magufuli aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wananchi, Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma, akirejea kutoka kwenye ziara ya kikazi mikoa ya Geita, Shinyanga na Tabora.

“Hakuna chakula cha bure sitatoa chakula kwenye wilaya yeyote, wilaya itakayopata njaa, mkuu wa wilaya na yeye ataondoka pia na viongozi ambao wanazembea kuwahamasisha wananchi kufanyakazi.

Usiyefanya kazi usile, hakuna cha bure. Asiyefanya kazi na asile. Fedha tunayopata ikaendelee kujenga miradi ya SGR (Reli ya Kisasa),” alisema.

“Kazi ya serikali kujenga hospitali, kununua ndege, dawa, reli na mengine ya maendeleo. Kujilisha ni kazi yako, si kazi ya serikali,” alisema Rais Magufuli.

Alisema pamoja na kuona maeneo kadhaa ya wilayani humo, yakiendelea kuwa na mvua, hakuna kilimo kinachoendelea.

“Ukienda Morogoro utakuta kinamama wamepanga viazi. Bahi kuna mvua, lakini sioni mkilima. Nimeshangaa, mama wa miaka 59 anaomba ekari tatu, alime, nilidhani wakuniomba ni kijana wa miaka 18, tena mkampe kesho huyu mama.”

Kadhalika, akiwa eneo la Manyoni, mkoani Singida, Rais Magufuli aliwataka wananchi kulima ili kujiongezea kipato.

“Mvua hazina kusubiri, zinaonyesha tulime, barabara hizi zitaleta faida iwapo tutazifanyia kazi, mazao yenu yataliwa maeneo yote sababu barabara ipo,” alisema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli alisema wakati mataifa mengine wananchi wao wakijifungia ndani kwa ajili ya corona, ni wakati wa Tanzania kufanya kilimo na kwamba viongozi wa eneo hilo wawahamasishe watu kufanya kazi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dk. Fatuma Mganga, alisema mapato yameongezeka kutoka Sh. milioni 500 hadi Sh. bilioni moja.

Alisema ongezeko hilo limefanya ujenzi wa sekondari kwenye kata mbili ambako hazikuwapo awali, kujengwa.

“Kata ya Nondwa tayari watoto wanasoma na kata ya Mpinga tunamalizia madarasa, tunatarajia hadi Februari yatakuwa yamekamilika,” alisema Dk. Mganga.

Aliongeza kuwa mapato ya ndani ya halmashauri hiyo, yamewezesha kutoa mikopo kwa vikundi 33 na kutoa ajira kwa makundi maalum.

“Madarasa 12 yanajengwa kwa wanafunzi waliokosa ambao wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza hadi mwezi ujao wataingia darasani.”



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Rais Magufuli Awasisitiza Wananchi Kulima, Kuchapa Kazi...."Usiyefanya kazi usile, hakuna cha bure"
Rais Magufuli Awasisitiza Wananchi Kulima, Kuchapa Kazi...."Usiyefanya kazi usile, hakuna cha bure"
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwZ_veNPXIyg64WalJNVT5iJSdh1WlfesSpLIhZbDT-4ABbKACRjc9ZhpalrJRAHlKfJL6K6c0DvW4TqE4b9qygjey-cGg498zaOiu3m-hyH1ldPwuGMhPGSGmm1pl5UHkv9RPKLJTd-Uv/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwZ_veNPXIyg64WalJNVT5iJSdh1WlfesSpLIhZbDT-4ABbKACRjc9ZhpalrJRAHlKfJL6K6c0DvW4TqE4b9qygjey-cGg498zaOiu3m-hyH1ldPwuGMhPGSGmm1pl5UHkv9RPKLJTd-Uv/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/rais-magufuli-awasisitiza-wananchi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/rais-magufuli-awasisitiza-wananchi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy