MABOSI YANGA WATAJA KILICHOBUMISHA DILI LA BWALYA KUSAJILIWA
HomeMichezo

MABOSI YANGA WATAJA KILICHOBUMISHA DILI LA BWALYA KUSAJILIWA

UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kuwa ulikuwa kwenye mpango wa kuinasa saini ya kiungo chaguo la kwanza la Didier Gomes ndani ya kikosi cha S...


UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kuwa ulikuwa kwenye mpango wa kuinasa saini ya kiungo chaguo la kwanza la Didier Gomes ndani ya kikosi cha Simba, Rarry Bwalya ila dili hilo lilibuma kutokana na kuhofia kupigwa mkwanja mrefu.

Bwalya akiwa na Simba chini ya Kocha Mkuu, Gomes ambaye ni mrithi wa mikoba ya Sven Vandenbroeck ambaye alibwaga manyanga ndani ya Simba, Januari 7 ameanza kikosi cha kwanza kwenye mechi zote tatu.

Ilikuwa mbili za Simba Super Cup na moja ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Dodoma Jiji, kabla ya kuibukia Simba alikuwa anatajwa kuwa kwenye mazungumzo na Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Cedric Kaze.

Injinia Hersi Said, Mkurugenzi wa Kampuni ya GSM ambao ni wadhamini wa Yanga ameweka wazi kuwa walikuwa kwenye mazungumzo na nyota huyo ila wakamkosa kwa kuwa waliamua kuachana naye.

 “Wakati wa usajili tiulikuwa na hesabu za kumsajili pia Larry Bwalya kwa kuwa tulifanya nae mazungumzo kwenye hatua za mwanzo ila ofa kutoka klabuni kwao ilikuwa kubwa na tuliiona haiendani na bajeti yetu ya usajili.


“Wakati tunamtaka sisi alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja ambao tulitakiwa kuuvunja kwa kulipia vipengele vitatu ambavyo vilikuwa kwenye mkataba wake ambavyo ni fedha ya uhamisho ambayo ingeenda kwa klabu yake,fedha ya kusaini mchezaji ambayo ingeingia moja kwa moja kwa mchezaji na fedha ya wakala.

"Kutokana na mwendo huo kuwa mrefu tuliiona kwamba ni jambo ambalo huenda tungepigwa kwa kuwa ilikuwa ni fedha ndefu.

“Hatujutii kumkosa Bwalya kwa kuwa si mchezaji wetu na bado tunaongoza ligi,” amesema Hersi.

Yanga ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 44 baada ya kucheza jumla ya mechi 18, Simba yenye Bwalya ipo nafasi ya pili na pointi 38 baada ya kucheza jumla mechi 16.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: MABOSI YANGA WATAJA KILICHOBUMISHA DILI LA BWALYA KUSAJILIWA
MABOSI YANGA WATAJA KILICHOBUMISHA DILI LA BWALYA KUSAJILIWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiZIDrngqoP02pGh7I-BipTuxmI6Aa-xyi9UlvZTJ7u_jEytVKe5cndgQ40BA8zW-oe81BnIbCZib2yfexPdkiph1p2EPeHUkZPTHSubQCuB8ZvF6fytUC-18QSUoqnKw87nJ4Y_LlbQsk4/w640-h558/Bwalya+na+Ruvu.PNG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiZIDrngqoP02pGh7I-BipTuxmI6Aa-xyi9UlvZTJ7u_jEytVKe5cndgQ40BA8zW-oe81BnIbCZib2yfexPdkiph1p2EPeHUkZPTHSubQCuB8ZvF6fytUC-18QSUoqnKw87nJ4Y_LlbQsk4/s72-w640-c-h558/Bwalya+na+Ruvu.PNG
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/mabosi-yanga-wataja-kilichobumisha-dili.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/mabosi-yanga-wataja-kilichobumisha-dili.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy