Corona Haijaathiri Upatikanaji Wa Mafuta-Waziri Kalemani
HomeHabari

Corona Haijaathiri Upatikanaji Wa Mafuta-Waziri Kalemani

Zuena Msuya Dar es Salaam, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amewatoa hofu watanzania kwa kusema kuwa tishio la virusi vya ugonjwa ...

Waziri Mkuu Atoa Rai Kwa Waliopata Ufadhili Wa Mafunzo Ya Ufundi
BREAKING: Rais Samia Afanya Uteuzi wa Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Jiji, Manispaa , Miji na Wilaya
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo August 2


Zuena Msuya Dar es Salaam,
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amewatoa hofu watanzania kwa kusema kuwa tishio la virusi vya ugonjwa wa corona halijaathiri upatikanaji wa mafuta nchini.

Aidha kuna ziada ya mafuta itakayotumika zaidi ya siku 30 na bado meli zinaendeleapakuwa mafuta bandarini.

Dkt. Kalemani alisema hayo Jijini Dar es Salaam, wakati wa ziara ya kutembelea bandari ili kujiridhirisha kama kuna mafuta ya kutosha kukidhi mahitaji yanayohitajika nchini, kwakuwa nchi imeingia Uchumi wa Kati na miradi mingi mikubwa inaendelea kutekelezwa.

Alisema Tanzania imejipanga vizuri katika suala la upatikanaji wa mafuta, pia aliwatoa hofu watanzania kuwa serikali inaendelea vizuri katika sekta hiyo kwani mpaka sasa, hakuna kiwango cha mafuta kilichopungua tangu kutangazwa kwa uwepo wa ugonjwa huo duniani kote.

Alisema kwa sasa, nchi ina mafuta mengi na ya kutosha, pia ziada ya lita Milioni 209 kwa mafuta Petroli, mafuta ya Diseli lita Milioni 121, Mafuta ya Taa lita laki 6, na Mafuta Ndege lita Milioni 18, ambayo yatatosha kutumika kwa zaidi ya siku 30 zijazo na bado meli zinaendelea kupakuwa mafuta bandarini: Leo kuna meli inapakua Tani 38 za Mafuta.

Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuna  mafuta ya kutosha siku zote ili miradi mikubwa ya kitaifa inayoendelea kutekelezwa kama vile ya SGR, Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere, Miundombinu ya Barabara, Maji na mingine mingi isikwame kwa kukosa mafuta kutokana na ugonjwa huo.

“Ninawahakikishia watanzania kwa niaba ya serikali kuwa mafuta yapo na yataendelea kuwepo, tumshukuru Rais wetu, Dkt. John Magufuli  kwa msimamo wake thabiti kwani anatuwezesha kufanya kazi usiku na mchana, hivyo hatutaweza kuathirika kwa yanayosemwa, tumekaa na wadau pamoja na wataalamu wetu tumeweka mpango na mikakati ya kuhakikisha mafuta yanapatikana muda wote”, alisema Dkt. Kalemani.

Kuhusu matumizi ya mafuta nchini, Dkt. Kalemani alisema kuwa matumizi yanaongezeka siku hadi siku, ambapo kwa sasa tunatumia Mafuta lita Milioni 5.7 ya Diseli, Petroli lita Milioni 4.6, Taa lita zaidi ya laki moja, na Ndege lita zaidi ya laki 6.

Aidha alisema kuwa, matumizi ya mafuta ya Taa yamepungua kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya umeme wa Gridi ya Taifa katika shughuli nyingi za kiuchumi na kijamii vijijini.

Dkt. Kalemani alifafanua kuwa, Mwaka jana nchi ilikuwa na jumla ya mafuta ya ziada ya lita Milioni 325, mwaka huu kuna ziada ya lita Milioni 412, hivyo amewataka wataalamu wanaosimamia sekta hiyo kuhakikisha kiwango cha upatikanaji wa mafuta kinaongezeka zaidi.

Hata hivyo alisisitiza kuwa licha ya kuwepo kwa bandari, lazima kuendelea kupima na kuongeza uwezo wa bandari hizo nchini, ambapo kwa sasa imeongezeka bandari ya Tanga na Mtwara.

“Mpango mathubuti wa serikali ni kuangalia uwezekano wa kuongeza bandari kavu au maghala ya kuhifadhi mafuta katika Mikoa ya Mwanza, Kigoma na Kagera zitakazotumika kuhifadhi mafuta ya takayosafirishwa nje ya nchi”, alisisitiza Dkt. Kalemani.

Katika hatua nyingine, aliwataka wawekezaji kuja kufanya utafiti na kuwekeza katika sekta ya mafuta, kwa kuwa bei ya mafuta katika soko la Duniani inaendelea kuongezeka ikilinganishwa  na miaka ya nyuma, na kueleza kuwa mwaka jana Pipa la mafuta ghafi lilikuwa Dola 50, ambapo kwa sasa ni Dola 57, Mafuta safi ilikuwa Dola 278, na sasa ni wastani wa Dola 446.

Katika ziara hiyo alitoa onyo kwa baadhi ya watanzania kuacha tabia ya kuhujumu miundombinu ya mafuta, ikitokea mtu amekamatwa kwa kosa hilo ahukumiwe kama wahujumu uchumi wengine kulingana na sheria za nchi: Pia Wataalamu pamoja na Timu ya Ulinzi na Usalama kuendelea kulinda na kusimamia miundombinu hiyo kwa maslahi mapana ya nchi na watanzania kwa ujumla.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Corona Haijaathiri Upatikanaji Wa Mafuta-Waziri Kalemani
Corona Haijaathiri Upatikanaji Wa Mafuta-Waziri Kalemani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh0ROzIbyHrUwNmrg0XVnbyBW6V84Jc0hQUIi8dgyWwWHlKPTO5b7kF00OHPHvx_B4i6UyhCQo-us6g_sQkGTBx8c79jdmUsjA1fAc2fuVPBa_xxkSzEzpdEL0emNrlvc4UAo4NmuqUu29D/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh0ROzIbyHrUwNmrg0XVnbyBW6V84Jc0hQUIi8dgyWwWHlKPTO5b7kF00OHPHvx_B4i6UyhCQo-us6g_sQkGTBx8c79jdmUsjA1fAc2fuVPBa_xxkSzEzpdEL0emNrlvc4UAo4NmuqUu29D/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/corona-haijaathiri-upatikanaji-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/corona-haijaathiri-upatikanaji-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy