Kimenuka Geita!! WAGANGA WA KIENYEJI 32 WAKAMATWA WAKIHUSISHWA NA MAUAJI YA ALBINO NA VIKONGWE!!
HomeHabariKitaifa

Kimenuka Geita!! WAGANGA WA KIENYEJI 32 WAKAMATWA WAKIHUSISHWA NA MAUAJI YA ALBINO NA VIKONGWE!!

wa Geita limewakamata waganga wa kienyeji  32 wanaopiga ramli chonganishi katika msako uliofanywa hivi karibun...

PAC yaagiza Wasira aondolewe kwenye nyumba anayoishi
Bomu lajeruhi watano
Kamamati za Bunge zawagwaya kina Chenge, Ngeleja



wa Geita limewakamata waganga wa kienyeji  32 wanaopiga ramli chonganishi katika msako uliofanywa hivi karibuni ili kuhakikisha mauaji ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi yanakomeshwa kabisa.


Akizunguza na waandishi wa habari baada ya kufanya msako na kuwakamata waganga hao kamanda wa polisi mkoa wa Geita Sacp Joseph Konyo amesema waganga hao wamekamatwa wakiwa na vifaa mbalimbali ambavyo ni matunguri na ngozi  za wanyama kama vile simba chui na nyati vikiwa vimekaushwa.
 
 
 Kamanda  Konyo mesema sasa wakati umefika wa kuhakikisha mauaji yanayotokana na imani potofu za kishirikina yanakomeshwa na ili kuyakomesha watu wa kwanza kudhibitiwa ni waganga wa kienyeji wanaofanya shughuli zao pasipo kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa na nchi.
 
Kamanda Konyo amesema upo ushahidi wa wazi unaonyesha mahusiano ya karibu ya mauaji haya ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi na waganga wa kienyeji kwani ndio wahusika wanaoagiza viungo vya Albino na ndio hao wanaopiga ramli za uongo kuonyesha kuwa vikongwe hasa wanawake ndio wachawi.
 
Ameongeza kuwa jeshi la Polisi haliwezi  kuhangaika na watu wengine wakati huku waganga ndiyo wanaosababisha mauaji hayo ya walemavu wa ngozi  na vikongwe  huku wakisababisha wananchi kuacha kufanya shughuli zao za kila siku
 
Kamanda Konyo amesema serikali haiwezi kuvumilia waganga wa namna hii wanaoipotosha jamii hivyo msako huu utaendeshwa katika mikoa yote Tanzania bara ili kubaki na jamii salama isiyokuwa na vitisho vya mauaji ya kikatili kama haya.
 
Baadhi ya wananchi mkoa wa Geita wameipongeza hatua ya serikali kuanza sasa kuwachukulia hatua watuhumiwa wote wanaopatikana na tuhuma za mauaji yanayotokana na mila potofu na ushirikina.

Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Kimenuka Geita!! WAGANGA WA KIENYEJI 32 WAKAMATWA WAKIHUSISHWA NA MAUAJI YA ALBINO NA VIKONGWE!!
Kimenuka Geita!! WAGANGA WA KIENYEJI 32 WAKAMATWA WAKIHUSISHWA NA MAUAJI YA ALBINO NA VIKONGWE!!
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgJjE7i6W4LEomTfmwVjtD8v1BSBTIzHaghI1NaqVpt3DdqcmKeFpNRl0R3p5_EC1D0j8e05ybPW3YO2TnqbTWgdM7LTpv-smOUEidjUF63flGxikpN5TtoKUB-8bGzdkU_UBs1MOcYXmy9/s1600/VURUGUMTWARA4.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgJjE7i6W4LEomTfmwVjtD8v1BSBTIzHaghI1NaqVpt3DdqcmKeFpNRl0R3p5_EC1D0j8e05ybPW3YO2TnqbTWgdM7LTpv-smOUEidjUF63flGxikpN5TtoKUB-8bGzdkU_UBs1MOcYXmy9/s72-c/VURUGUMTWARA4.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/kimenuka-geita-waganga-wa-kienyeji-32.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/kimenuka-geita-waganga-wa-kienyeji-32.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy