Dr. Slaa na Makada 3 wa CHADEMA Kupelekwa Kortini na Polisi Kwa Tuhuma za Kumpiga Kagenzi ambaye Alikuwa Mlinzi Wake
HomeHabariKitaifa

Dr. Slaa na Makada 3 wa CHADEMA Kupelekwa Kortini na Polisi Kwa Tuhuma za Kumpiga Kagenzi ambaye Alikuwa Mlinzi Wake

JESHI la Polsi Kanda Maalum ya Dar es Salaam lipo katika hatua ya mwisho katika kukamilisha ushahidi ili kumfikikisha mahakaman...




JESHI la Polsi Kanda Maalum ya Dar es Salaam lipo katika hatua ya mwisho katika kukamilisha ushahidi ili kumfikikisha mahakamani Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dokta Wilbrod Slaa pamoja na makada wa chama hicho.


Akizungumza na waandishi wa Habari jana mchana Jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Kanda maalum Dar es Salaam Suleiman Kova alitaja sababu ya kumfikisha mahakani katibu huyo wa CHADEMA na makada wake kuwa ni vitendo vinavyodaiwa ni vya kinyama alivyofanyiwa mlinzi wake vya kumteka, kumpiga na kumlazimisha kutaja watu wanaomtuma kumuua Dr.Slaa
 

Jeshi hilo  limesema kwa sasa linawashikilia makada watatu wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini ambao ni Boniface Jacob (miaka 32) mkazi wa Ubungo Kisiwani ambaye pia ni Diwani wa kata ya Ubungo kupitia chama hicho, Hemed Ally Sabula (miaka 48) mkazi wa Tandale kwa Tumbo ambaye anadaiwa ni Afisa Usalama wa chama hicho Taifa.






Mbali na hao pia Kamishna Kova alimtaja kada mwingine anayeshikiliwa kuwa ni Benson Mramba (miaka 30), mkazi Tabata Kisukulu ambaye ni Afisa Utawala wa CHADEMA.


Kamishna Kova alibainisha kuwa ushahidi wao utakapokamilika mafaili yao yatafikishwa kwa Wakili wa Serikali ili hatua zichukuliwe. 


Akizungumzia sakata la mlinzi Kagenzi, Kova alisema kuwa kwa sasa wanamalizia kazi ya kukusanya ushahidi kutoka CHADEMA ambao wanamtuhumu bwana Kagenzi ambaye anafanya ushirikiano na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Philip Mangula na Afisa Usalama wa Taifa Mkoa wa Kinondoni kuandaa mpango wa kutaka kumuwekea sumu Dokta Slaa.


Kesi hiyo kwa mara ya kwanza ilifika Polisi tarehe 8 mwezi huu majira ya saa 11 jioni katika kituo cha Polisi cha Oysterbay kupitia kwa wakili wa CHADEMA anayetambulika kwa jina la john Mallya akiambatana na mtuhumiwa Khalid Kagenzi ambaye ni mkazi wa Tandale kwa Tumbo ambapo Wakili huyo aliiambia polisi kwamba alimleta mtuhumiwa baada ya kuagizwa na Dokta Slaa ili kutoa malalamiko kwa niaba yake.


Katika maelezo yake anadai Wakili huyo kuwa uongozi wa CHADEMA ulikuwa umechukuwa hatua mbalimbali dhidi ya Kagenzi ikiwemo kumbana na kujiridhisha kuwa anahusika na mipango ya kimauaji.


Kwa mujibu wa Kamishna Kova, katika mahojiano walibaini kuna vitendo vya kinyama ambavyo mlinzi huyo wa Dokta Slaa amefanyiwa na makada wa CHADEMA baada ya Jeshi hilo kumkuta akiwa na majeraha mbalimbali katika mwili wake.
 



 




Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Dr. Slaa na Makada 3 wa CHADEMA Kupelekwa Kortini na Polisi Kwa Tuhuma za Kumpiga Kagenzi ambaye Alikuwa Mlinzi Wake
Dr. Slaa na Makada 3 wa CHADEMA Kupelekwa Kortini na Polisi Kwa Tuhuma za Kumpiga Kagenzi ambaye Alikuwa Mlinzi Wake
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqoHPZpwQs5WSnVwbFoRCKl18QbRXsHTj5JleFC8fiXqe65w7vVkNaglCc7u2fQMLVVZAGLxkms7TAUayaAqd4Df6frMIFf3U1fVaEZOLSFtjldiE90yDw6AcS7aY4WAwbQHy4CQkkJjXe/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqoHPZpwQs5WSnVwbFoRCKl18QbRXsHTj5JleFC8fiXqe65w7vVkNaglCc7u2fQMLVVZAGLxkms7TAUayaAqd4Df6frMIFf3U1fVaEZOLSFtjldiE90yDw6AcS7aY4WAwbQHy4CQkkJjXe/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/dr-slaa-na-makada-3-wa-chadema.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/dr-slaa-na-makada-3-wa-chadema.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy