BINTI aliyefahamika kwa jina moja la Ashura, anayedaiwa kuwa ni mke wa mtu, hivi karibuni alimtoroka bwana’ke na kuonekana akiji...
BINTI aliyefahamika kwa jina moja la Ashura, anayedaiwa kuwa ni mke wa mtu, hivi karibuni alimtoroka bwana’ke na kuonekana akijiachia hovyo na wanaume watano tofauti katika Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar es Salaam kulipokuwa na onyesho la Bendi ya Taarabu ya Mashauzi Classic.
Akionekana kuwa ‘vizuri’ kichwani, kwa kiburudisho alichopata usiku mnene, binti huyo alionyesha umahiri mkubwa wa kukata mauno kiasi cha kuwavutia wanaume ambao kila mmoja alitaka kuwa naye karibu kiasi cha kumfanya kuwa bize kwa kila wimbo kulazimika kucheza na wanaume tofauti.
Hata hivyo baadhi ya mashabiki wa bendi hiyo walisema mrembo huyo alitia aibu kwani kuna wakati alicheza hadi nguo zake za ndani zikawa zinaonekana.
COMMENTS