Malabo wageuka Uwanja wa Vita
Polisi wakijaribu kutuliza ghasia
HomeHabariKimataifa

Malabo wageuka Uwanja wa Vita

Polisi wakijaribu kutuliza ghasia Nusu fainali za pili za michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Afcon kati ya Gh...




Nusu fainali za pili za michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Afcon kati ya Ghana na wenyeji Equatorial Guinea zinaelezwa kama "ukanda wa vita" baada ya mchezo huo kusitishwa kwa zaidi ya dakika 30 kwa sababu ya ghasia za mashabiki.

Mashabiki kutoka majukwaani waliwarushia chupa za maji wachezaji, na kulazimisha mashabiki wa Ghana kutafuta mahali pa kusitiri maisha yao nyuma ya goli, polisi wa kuzuia ghasia na helikopta iliruka juu ya uwanja kuwatuliza mashabiki lakini hawakufanikiwa.

"Ni kama sasa uwanja wa vita," kiliandika chama cha mpira cha Ghana(GFA) katika ujumbe wake wa tweeter, kikidai kuwepo kwa vitendo vya "kinyama na uharibifu" na "mashambulio ya vurugu kwa jambo lisilo na sababu" yalifanyika ndani ya uwanjani.

Wakati mchezo unarejea, Ghana tayari ilikuwa imefunga magoli 3-0 na kutinga fainali dhidi ya Ivory Coast itakayochezwa Jumapili. Kufika hatua hiyo Ivory Coast, iliifunga DR Congo 3-1 katika nusu fainali ya kwanza iliyochezwa Jumatano.


Watazamaji wakijaribu kukimbia


Vurugu zilikithiri katika kipindi cha pili cha mchezo kati ya Ghana na Equatorial Guinea.

Ushindi huo wa Ghana haukuwafurahisha mashabiki wa timu mwenyeji, ambao walikuwa na matumaini makubwa kuona timu yao inacheza fainali ya Jumapili dhidi ya Ivory Coast.

Ghana ilianza kujipatia magoli yake kupitia kwa Jordan Ayew akifunga katika dakika ya 42 kwa njia ya penalti, Wakaso Mubarak dakika ya 45 na Andre Ayew alikipigilia msumari wa moto katika dakika ya 75.

Goli hilo la tatu ndilo lililokuwa limezidisha fujo kiwanjani kwa mashabiki wa Equatorial Guinea kuwarushia chupa za maji wachezaji kiasi cha mpira huo kusimamishwa kwa muda mrefu.

Kwa matokeo hayo Ivory Coast na Ghana ndizo zitakazocheza fainali za Afcon kwa mwaka 2015 siku ya Jumapili zinazofanyika nchini Equatorial Guinea na kutangazwa moja kwa moja na BBC.

Lakini mchezo huo utatanguliwa na ule wa Jumamosi kutafuta mshindi wa tatu kati Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo dhidi ya Equatorial Guinea.
 
Chanzo BBC
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Malabo wageuka Uwanja wa Vita
Malabo wageuka Uwanja wa Vita
http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/304/amz/worldservice/live/assets/images/2015/02/05/150205220336_ghana_can_304x171_afp_nocredit.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/02/malabo-wageuka-uwanja-wa-vita.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/02/malabo-wageuka-uwanja-wa-vita.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy