SI siri tena! Staa wa wimbo wa Ndakushima, Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ kwa sasa ameamua kukiri wazi kuwa ananogewa na penzi la Wema Se...
SI siri tena! Staa wa wimbo wa Ndakushima, Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ kwa sasa ameamua kukiri wazi kuwa ananogewa na penzi la Wema Sepetu ‘Madame’.
Staa wa wimbo wa Ndakushima, Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ akiwa na Wema Sepetu ‘Madame’.
Akizungumza
na paparazi wetu Februari 11, mwaka huu maeneo ya Kinondoni jijini Dar
es Salaam, Dimpoz alisema anawashangaa sana watu kuendelea kumsakama juu
ya uhusiano wake na Madame wakati yeye anafahamu shemeji yake kwa
Nasibu Abdul ‘Diamond’ ni Zarina Hassan ‘Zari’ kwa sasa.
“Nashindwa
kuelewa kuna watu wamekuwa wakinitumia ujumbe eti Diamond atanimaindi
kwa ukaribu wangu na Wema, Diamond atanichukia wakati ninavyojua demu
wake kwa sasa ni Zari? Niwaambie tu ukaribu wa mimi na Wema ulianza
tangu zamani alipokuwa na Diamond,” alisema Dimpoz.
Wakiwa kwenye pozi la kimahaba.
Mahabati
ya Dimpoz na Wema yalianza kuonekana laivu juzikati wakati wawili hao
walipokuwa nchini Afrika Kusini wakidai kuna ‘project’ ya ngoma mpya ya
mwanamuziki huyo waliyokuwa wakiifanya kisha picha zilizowaonesha wakiwa
kimahaba zikavuja na kuzua gumzo mitandaoni.
COMMENTS