Aliye kuwa Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steven Nyerere hivi karibuni aliibua miguno baada ya kumganda kifuani mama wa msani...
Aliye
kuwa Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steven Nyerere hivi karibuni aliibua
miguno baada ya kumganda kifuani mama wa msanii Elizabeth Michael,
Lucresia Karugila huku akionekana kutotaka kubanduka mwilini mwa mama
huyo.
Tukio
hilo lililowafanya watu wabaki wakiwa wamepigwa butwaa, lilijiri ndani
ya Hoteli ya Landmark jijini Dar kulikokuwa na uzinduzi wa kitabu cha
Marehemu Steven Kanumba kiitwacho The Great Follen Tree.
Awali,
waalikwa kwenye sherehe hiyo waliinuka na kwenda kucheza wimbo wa
Christian Bella wa Nani Kama Mama lakini katika hali ya kushangaza,
msanii huyo alikwenda na kumvaa mama Lulu kwa staili ya kumkumbatia
kisha kumganda kwa sekunde kadhaa hali iliyoibua maneno.
“Jamani
jamani hebu mtazameni Steve alivyoganda kifuani kwa Mama Lulu, dah!
Huyu jamaa ana balaa kweli, hata kama ni kucheza au ni salamu ndo
amgande mama wa watu vile?’’ alisikika akihoji mmoja wa wadau.
COMMENTS