MAMBO si mambo! Tayari mimba ya muigizaji Aunt Ezekiel imeanza kumtibua baada ya nyota huyo kushindwa kufanya baadhi...
Mose Iyobo akimsaidia kuvaa kiatu muigizaji maarufu Bongo, Aunt Ezekiel.
Kwa
mujibu wa chanzo chetu, kutokana na tumbo kuwa kubwa, Aunt kwa sasa
hawezi kufunga viatu vyake, kufua, kuosha vyombo na hata akitaka kwenda
toileti inabidi apewe kampani na mtu.“Mh! Jamani Aunt hata kuinama ni mtihani sasa sijui kama ni kujidekeza au nini maana anapokuwa karibu na bebi wake ndiyo usiseme ni full kudeka anasema akiinama anaumia jamani?“Eti sasa hivi shosti wake Wema Sepetu na bebi wake Mose Iyobo ndiyo wamekuwa wakifanya kazi ya ziada kumsaidia kila kazi nyingi anazoshindwa,” kilisema chanzo hicho.
“Jamani hivi niiname nimkunje mtoto wangu bila sababu za msingi na watu wapo ambao wanaweza kunisaidia kwa nini nijiumize, acheni nisaidiwe,” alisema Aunt.Kwa upande wake, Mose ambaye inaaminika kuwa ndiye mhusika wa mimba hiyo ya Aunt alipozungumza na mwanahabari wetu, alijisifu na kusema anafurahi kuwa baba bora wa Aunt.
COMMENTS