Wapiganaji wa ISIS wakiua kundi la watu kwa risasi©RT Kundi hatari linalodai kutetea na kufuata haki za dini ya kiislamu linalo...
Wapiganaji wa ISIS wakiua kundi la watu kwa risasi©RT
Kundi
hatari linalodai kutetea na kufuata haki za dini ya kiislamu
linalopigana nchini Iraq na Syria la Islamic State limewanyonga
wapiganaji wake wa kigeni zaidi ya120 kufuatia wapiganaji hao kutaka
kuondoka na kurudi makwao na kuachana na kundi hilo.
Wapiganaji
waliouwawa ni waliokuwa wakitumikia kundi hilo katika mji wa Raqqa
nchini Syria walikamatwa wakijaribu kutoroka kurudi makwao kama chanzo
cha taarifa hii kilipozungumza na mwandishi wa The Financial Times ambaye
amedai watu wanaopinga vitendo vya ISIS na utawala wa Rais Bashar
al-Assad amesema watu waliouwawa walikuwa wakijaribu kutoroka baada ya
ISIS kutoa mwongozo mpya wa wapiganaji wake katika kuwazuia kukimbia.
Ingawa
kuna wapiganaji wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani wanaojiunga na
kundi hilo kwakuhadaiwa kwamba ISIS itawasaidia kuielewa vyema dini ya
kiislamu na mara baada ya kujiunga wanajikuta walidanganywa na matokeo
yake wanajiingiza katika vitendo vya kikatili vya mauaji vinavyofanywa
na wapiganaji wa kundi hilo na kutaka kujiondoka kitu ambacho
hakiwezekani. Aidha taarifa hiyo inasema wapiganaji mara wanapojiunga
hutakiwa kupigana na kutojitoa katika kundi hilo la linalodai kufuata
misingi ya dini na kupokea vitisho kutoka kwa wapiganaji wengine wa ISIS
kwamba watauwawa endapo watajaribu kutoroka.
Kumekuwa na kundi kubwa
la vijana na watu wa makamo sehemu mbalimbali duniani ambao huadaiwa na
kundi hilo la ISIS likiwashawishi kwa njia ya mtandao au kupitia
wawakilishi wao waliopo nchi mbalimbali kwa kificho ili kwenda kujiunga
nao katika mapigano ili kuendeleza ama kudumisha dini ya Kiislamu na
matokeo yake hujikuta wamehadaiwa na kujiingiza kwenye mauaji yasiyo na
hatia ya kuua hata watoto kwakisingizio cha dini, kitendo ambacho
kimekuwa kikipingwa na waumini mbalimbali wa dini ya kiislamu na dini
nyingine duniani.

COMMENTS