JK: Uhusiano na Msumbiji utaendelea kudumishwa
Raisi Jakaya Kikwete
HomeHabariKitaifa

JK: Uhusiano na Msumbiji utaendelea kudumishwa

Raisi Jakaya Kikwete RAIS Jakaya Kikwete amesema uhusiano wa Tanzania na Msumbiji ni wa kipekee na kindugu hivyo utaendelea kudumishwa...

Japan yachangia mil 160/- shule ya msingi Kakuni
Sifa za ziada za Padri feki
Kimenuka Geita!! WAGANGA WA KIENYEJI 32 WAKAMATWA WAKIHUSISHWA NA MAUAJI YA ALBINO NA VIKONGWE!!
RAIS Jakaya Kikwete amesema uhusiano wa Tanzania na Msumbiji ni wa kipekee na kindugu hivyo utaendelea kudumishwa kwa manufaa ya pande zote mbili.
Kikwete alisema hayo juzi muda mfupi baada ya kuwasili mjini Maputo kwa ajili ya kuhudhuria kuapishwa kwa Rais wa Msumbiji, Filipe Nyusi na kupokea taarifa ya Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Shamsa Nyanduga.

Alisema Tanzania na Msumbiji ni washirika na zina ushirikiano, hivyo hauwezi kupotea hasa wakati huu ambapo kuna ugunduzi wa mambo mazuri pande zote, ikiwa pamoja na suala la gesi.
“Tuna ushirikiano wa muda mrefu na Msumbiji, hawa ni ndugu na rafiki zetu tumetoka nao mbali na hata chama cha Frelimo kimeundiwa Dar es Salaam, ni rahisi kuendeleza ushirikiano nao katika masuala mbalimbali ya maendeleo na kudumisha uhusiano wetu mzuri,”’ alisema Balozi Nyanduga akitoa taarifa ya ubalozi kwa Rais Kikwete, alisema uhusiano kati ya Tanzania na Msumbiji ni imara na wa kindugu.

Aidha, Balozi Nyanduga alisema uhusiano kati ya vyama tawala vya CCM na Frelimo ni mzuri na kuongeza kuwa katika kuimarisha uhusiano zaidi, Rais Nyusi alipoteuliwa na Frelimo kuwa mgombea urais, alifanya ziara ya kujitambulisha nchi za nje, kwa kuanzia na Tanzania kuonesha mchango wa Tanzania katika ukombozi wa Msumbiji.

Alisema viongozi wa ngazi mbalimbali wa serikali na CCM na Frelimo, wamekuwa wakitembeleana na kuna mafanikio makubwa ya uhusiano huo wa kisiasa. Lakini alisema uhusiano wa kiuchumi na kibiashara, bado ni mdogo, licha ya ujirani na muingiliano mkubwa wa wananchi pande zote.

Balozi Nyanduga alimweleza Rais kuwa licha ya sherehe hizo za kuapishwa Rais Nyusi, bendera za nchi hiyo zinapepea nusu mlingoti baada ya watu 79 kufa na 154 kulazwa hospitalini baada ya kunywa pombe ya kienyeji, iliyosadikiwa kutiwa sumu ya mamba katika mkoa wa Tete.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: JK: Uhusiano na Msumbiji utaendelea kudumishwa
JK: Uhusiano na Msumbiji utaendelea kudumishwa
http://www.habarileo.co.tz/images/resized/images/jakaya-mrisho-kikwete_300_173.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/jk-uhusiano-na-msumbiji-utaendelea.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/jk-uhusiano-na-msumbiji-utaendelea.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy