Serikali Kuleta Mabadiliko Makubwa Katika Sekta Ya Elimu Nchini
HomeHabari

Serikali Kuleta Mabadiliko Makubwa Katika Sekta Ya Elimu Nchini

SERIKALI imetangaza kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya Elimu hapa nchini  kuanzia Shule ya Msingi hadi Sekondari. Mabadiliko hayo...

Rais Samia Aitaka Wizara Ya Elimu Na Mafunzo Ya Amali Kufanya Mabadiliko Katika Sekta Ya Elimu
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo June 20
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo June 19


SERIKALI imetangaza kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya Elimu hapa nchini  kuanzia Shule ya Msingi hadi Sekondari. Mabadiliko hayo yamelenga kuwaandaa wanafunzi kujifunza kwa vitendo katika masomo ya kilimo, Sayansi kimu (Home Economics), Ufundi na biashara (Book-Keeping na Cormmerce).

Mafunzo hayo ya vitendo  yatawawezesha wanafunzi  kupata ujuzi wa  kukidhi matakwa ya ajira ikiwemo kwenye sekta ya kilimo, Utalii  na biashara.

Kupitia Mpango huo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeweka mipango ya kuwandaa Walimu kwa kuwapa mafunzo  endelevu kazini ili kuwapatia uwezo wa kuwafundisha wanafunzi vizuri.
 
Mkakati huo umetangazwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda (Mb) jana tarehe 4/5/2022 wakati akifungua mafunzo maalumu kwa walimu 322 wa masomo ya Mchepuo wa kilimo na Sayansi kimu kutoka mikoa ya yote ya Tanzania Bara na Zanzibar yanayofanyika Mkoani Morogoro.

 
Prof.  Mkenda amesema tayari Wizara hiyo imeanza kutoa kipaumbele kwa mafunzo ya walimu wa masomo hayo hapa nchini kwa kuwaongezea ujuzi na maarifa ya kwenda kuwafundisha wanafunzi ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
 

“Tunataka kuwandaa vijana ambao wataweza kuongeza ajira katika sekta ya kilimo, Biashara  na utalii ambao tayari umeshatangazwa nje ya nchi na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Filamu ya Utalii ya “ The RoyarTour.
 
Kwa Upande wake, Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt.  Aneth Komba, amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wa kitalaamu walimu wa masomo ya Sayansi kimu na Kilimo kwa kuwapa mbinu za ufundishaji, ujifunzaji na upimaji unaozingatia ujenzi wa umahiri.
 
Dkt. Komba alisema kuwa matokeo ya mafunzo hayo yatamuwezesha muhitimu wa masomo hayo kupata maarifa, stadi za kutenda na uelekeo wa kujitegemea kwa manufaa mapana ya jamii na Taifa kwa ujumla.

 
‘Mafunzo haya yanawajengea walimu hawa uwezo mkubwa  ambao watakwenda kuuambukiza kwa walimu wengine na baadae kwa walimu wanaowafundisha  ambao wataingia katika soko la ajira na wengine kuweza kujiajiri” amesema Dkt. Komba.
 

Kwa upande wa Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Hadija Mcheka, amesema kuwa mafunzo hayo yamekuja kwa wakati kutokana na kuwepo kwa upungufu mkubwa wa walimu wa masomo hayo na kwamba wataendelea kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kusaidia kuongeza idadi ya walimu wanafundisha masomo hayo hapa nchini.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Kuleta Mabadiliko Makubwa Katika Sekta Ya Elimu Nchini
Serikali Kuleta Mabadiliko Makubwa Katika Sekta Ya Elimu Nchini
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghDMsIHqbKJrGZlrMypQVdwWpDt9uQf7rtSU7nshQ5beMhvd2EJ2y1t2PMQm6ntzyjFNmkIMN675gswwcem-MPd0m3TxldP_-KJRIToInFJ6jKSGZYNuBo_chkP4ZJUP8_ohBTipTgL1ccNvYKcjpSGY3bPzrZwDEnOWSaVBcLjAvIJPFIgR9b3AxO4w/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghDMsIHqbKJrGZlrMypQVdwWpDt9uQf7rtSU7nshQ5beMhvd2EJ2y1t2PMQm6ntzyjFNmkIMN675gswwcem-MPd0m3TxldP_-KJRIToInFJ6jKSGZYNuBo_chkP4ZJUP8_ohBTipTgL1ccNvYKcjpSGY3bPzrZwDEnOWSaVBcLjAvIJPFIgR9b3AxO4w/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/serikali-kuleta-mabadiliko-makubwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/serikali-kuleta-mabadiliko-makubwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy